- Ukusanyaji za sahihi za BBI umeanza leo
- Ruto amesema sio lazima pawepo ushindani katika kura ya maoni
Naibu wa rais William Ruto ameshkilia kwamba bado kuna fursa ya mwafaka kupatikana kuhusu BBI ili kuepuka kura ya maoni itakayozua ushindani lichaya sahihi kuanza kukusanya siku ya jumatano kufanikisha marekebisho ya katiba .
Kupitia twitter Ruto amesema bado kuna uwezekano wa kuanda kura ya maoni ambayo sio lazima iwe na pande mbili za kunga mkono na kupinga .
Katika ujumbe wake amesema kwamba umoja ndio nguvu inayohitajika kukabiliana na mgogoro wa sasa wa janga la corona na kuboresha uchumi wan chi .
Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga siku ya jumatano wamezindua ukusanyaji wa sahihi za BBI katika ukumbi wa KICC .
Wakati wa hafla hiyo raia kenyatta alisisitiza kuhusu umuhimu wa handshake akisema mwafaka huo ulizuia Kenya kutumbukia katika mgawanyiko zaidi .
Even with the SIGNATURE launch there is still a real chance at CONSENSUS for a NON-DIVISIVE referendum that will give kenyans the opportunity to EXPRESS themselves without an US vs THEM, WIN vs LOSE contest. UNITY is the STRENGTH needed to fight COVID19 and organise the ECONOMY.
— William Samoei Ruto, PhD (@WilliamsRuto) November 25, 2020
Raila Odinga anaye alaisema masuala yanayohusu wananchi na hali ya uchumi yanaweza kushughulikiwa kupitia sheria na sera za serikali . Alikuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa ukusanyaji wa sahihi za BBI katika ukumbi wa KICC .
Kuhusu wadhifa ya msimamizi wa idara ya mahakama ambalo limekuwa donda sugu katika ripoti ya BBI Raila amesema jopo la uteuzi litampa rais majina ya watu watatu ambao yatatumwa bungeni kupigwa msasa na kisha moja kuteuliwa na rais .
" Hilo litavuruga vipi uhuru wa idara ya mahakama? Raila amesema
" Tumepitia mengi ya uhasama na siku ngumu na hata vipindi vya kubaguliwa na tunaweza kuona tunakotaka kwenda’
Amewahimiza wakenya kujitokeza kwa wingi na kutia saini zinazohitajika kufanikisha kura ya maoni ili kuirekebisha katiba .