Msimamo wa ANC

Mudavadi asifia BBI ,aunda kikosi cha kuipigia debe ripoti hiyo

Mudavadi asema chama chake sasa kinaunga mkono BBI

Muhtasari

 

  • Mudavadi amesifia mikakati iliyopendekezwa kulinda ugatuzi ,kutolewa kwa baraza la polisi na kulipa bunge la senate  nguvu zaidi
  •  Kwa sababu ya hatua hiyo ANC Imeunda kundi lake la kuipigia debe ripoti ya BBI .

 

 

Kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi

 Kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi  sasa amesema anaunga mkono kikamilifu  mapendekeo yaliyotolewa katika ripoti ya BBI na ataunga mkono kuandaliwa kwa  kura ya maoni .

 Mudavadi amesema  chama  chake kimepitia mapendekezo hayo ya BBI na  kuamua kwamba ni mazuri kwani masuala yote walioibua yameshughulikiwa .

Mudavadi amesifia mikakati iliyopendekezwa kulinda ugatuzi ,kutolewa kwa baraza la polisi na kulipa bunge la senate  nguvu zaidi

 Kwa sababu ya hatua hiyo ANC Imeunda kundi lake la kuipigia debe ripoti ya BBI .

 “ Tunataka kuzungumza na wakenya bila kutoa fursa ya watu kurushiana matusi  .wakenya wanafaa kupewa fursa ya  kujieleza.kwa hivyo tutazindua kundi letu kwanu hivi karibuni’ amesema Mudavadi

 Akizungumza katika makao makuu ya ANC Mudavadi amesema kulindwa kwa Nairobi kama kaunti ni hatua itakayoboresha ugatuzi .

 Amesema hatua hiyo  itawapa wakaazi wa jiji fursa ya kuwachagua watu bora kushughulikia mahitaji yao .

 Mudavadi amesema stakabadhi hiyo mpya inaonyesha kwamba mapendekezo yao yalitiliwa maanani .