- Ombeta alifanyiwa vipimo siku ya jumapili na matokeo yametolewa leo wakati kikao cha korti kilipotarajiwa kufanyika .
- Mwezi oktoba kesi hiyo iliahirishwa tena baada ya mtuhumiwa mmoja Chebuert kupatikana na corona .
Kesi ya mauaji ya wakili Willie Kimani imeahirishwa hadi jumanne baada ya mahakama kuambiwa kwamna wakili Cliff Ombeta ameambukizwa virusi vya Corona .
Ombeta anawaakilisha Fredrick Leliman na Stephen Cheburet, washtumiwa wawili katika esi hiyo ya mauaji .
Jaji Jessie Lessit ameelekeza kwamba Ombeta aitumie korto matokeo siku ya jumanne . Korti iliarifiwa kwamba Ombeta alitangamana na mteja mmoja huko malindi ambaye alipatikana na Corona na kulazwa hospitalini .
Ombeta alifanyiwa vipimo siku ya jumapili na matokeo yametolewa leo wakati kikao cha korti kilipotarajiwa kufanyika .
Mwezi oktoba kesi hiyo iliahirishwa tena baada ya mtuhumiwa mmoja Chebuert kupatikana na corona .
Kesi hiyo ilifaa kusikizwa kupitia njia ya kidijitali kutoka gereza la kamiti lakini Cheburet alisema alikuwa akiugua .
Watuhumiwa wote walikuwepo isipokuwa Cheburet ambaye aliitaka mahakama kuahirisha kikao hicho .Ombeta aliwasiliana naye kupitia zoom na kumuambia jaji Lessit kwamba amepimwa mara tano na vipimo vyote vilionyesha kwamna ana covid 19.