Kupambana na uhalifu

Chuo cha mafunzo ya DCI chaanzisha kozi mpya ya mafunzo ya uchunguzi wa uhalifu

DCI yaanzisha kozi mpya kuwapa ujuzi maafisa wake

Muhtasari
  •  Akiongoza uzinduzi wa kozi hiyo naibu mkurugenzi wa DCI Joseph shimala  amesema  kozi hiyo itakayowaleta pamoja maafisa 50 kutoka vitengo mbali mbali vya DCI itachukua muda wa wiki nane .
  •  Kulingana na Ashimala  maaafisa wa  usalama wana jukumu kubwa la kukabiliana na changamoto zote   wanazokabiliana nazo katika kutekeleza kazi  yao .

 

Baadhi ya maafisa wa DCI wakishiriki mafunzo

 Idara  ya DCI imeanzisha rasmi mafunzo ya kozi mpya kuhusu uchunguzi wa uhalifu katika chuo chake .

 Kozi hiyo maalum ya mafunzo kuhusu uchunguzi wa uhalifu  inalenga kuwapa  ujuzi maafisa hao kuweza  kutumia njia za kitaalam kukabiliana na kesi za uhalifu zinazohitaji ujuzi wa hali ya juu .

 Akiongoza uzinduzi wa kozi hiyo naibu mkurugenzi wa DCI Joseph shimala  amesema  kozi hiyo itakayowaleta pamoja maafisa 50 kutoka vitengo mbali mbali vya DCI itachukua muda wa wiki nane .

 Kulingana na Ashimala  maaafisa wa  usalama wana jukumu kubwa la kukabiliana na changamoto zote   wanazokabiliana nazo katika kutekeleza kazi  yao .

 Amesema  ni jambo la kusikitisha kwamba baadhi ya wahalifu hukimbilia mahakama kupewa bondi za kibinafasi baada ya kufanya makosa kwani hatua hiyo inazuia kupatikana kwa haki .