Hotuba ya Trump

Trump : Tulifanya tulichokuja kufanya

Trump alisema utawala wake ulifanya kile ulichotaka kufanya na mengi zaidi.

Muhtasari
  •  Katika video iliyowekwa youtube  Trump alisema ‘ Nilipigavana vita vikali na kukabiliana na mengi kwa sababi hiyo ndio sababu mlionichagua’
  •  Bwana Trump hajakubali hadi sasa matokeo ya uchaguzi wa novemba iliyopita baada ya kushindwa na Joe Biden wa chama cha Democrat .
Rais anayeondoka wa Marekani Donald Trump

Rais anayeondoka wa Marekani Donald Trump  ametoa hotuba yake ya kuiaga nchi baada ya miaka mine afisini akisema kwamba ‘Tumefanya tulichokja kufanya –na mengi  zaidi’

 Katika video iliyowekwa youtube  Trump alisema ‘ Nilipigavana vita vikali na kukabiliana na mengi kwa sababi hiyo ndio sababu mlionichagua’

 Bwana Trump hajakubali hadi sasa matokeo ya uchaguzi wa novemba iliyopita baada ya kushindwa na Joe Biden wa chama cha Democrat .

 

 Bwana  Biden   ataapishwa jumatano ili kuchukua hatamu za uongozi . wiki mbili zilizopita zimekuwa ngumu kwa Trump baada ya tofauti kubwa kuibuka miongoni mwa wafuasi wake  kutokana na uvamizi ulifanywa katika bunge  la Congress  na watu wanaomuunga mkono ili kuzuia wanachama wa bunge hilo kuidhinisha matokeo ya ushindi wa Biden .

" Ghasia za kisiasa ni shambulizi dhidi ya vyote tunavyoviamini kama wamarekani . Haziwezi kukubalika’ amesema Trump  katika ujumbe huo wa video  ambao hakumtaja mrithi wake kwa jina .

 Bunge la Congress lilipiga kura kumfurusha afisini Trump kwa madai ya ‘kuunga mkono maasi’  na sasa senate itaanza vikao vya kujadili hoja hiyo  na huenda akazuiwa kuwania  wadhfa wowote wa umma . Ni rais wa kwanza wa Marekani kupigiwa kura ya kutokuwa na imani mara mbili . Trump aliratibu baadhi ya mafanikio yake akisema alifaulu kuujenga uchumi wa Marekani kuwa thabiti .

 Anaondoka afisini huku kura za maoni zikionyesha kwamba ana uungwaji mkono wa asilimia 34 , kiwango cha chini sana kwa rais anayeacha maamlaka . Katika ujumbe huo wa dakika 20  Trump alisema utawala wake ulifanya  kile ulichotaka kufanya  na mengi zaidi.