Diplomasia

Hakuna ushahidi kwamba Kenya inaingilia masuala ya ndani ya Somalia-IGAD

Madai hayo yalisababisha mgogoro wa kidiplomasia kati ya Kenya na Somalia na kila nchi ikawaita nyumbani mabalozi wake .

Muhtasari
  •  Madai hayo yalisababisha  mgogoro wa kidiplomasia kati ya Kenya na Somalia na  kila nchi ikawaita nyumbani mabalozi wake .
  • Somalia imekuwa ikishikilia kwamba Kenya inaingilia masuala yake ya ndani kuifanya dhaifu 

 

 Kundi lililoteuliwa kuchunguza  madai ya omalia kwamba Kenya inaingilia masuala yake ya ndani  na kuyahami makundi ya wapiganaji  limesema hakuna usahidi kwamba Kenya inahusika na vitendo kama hivyo .

 Madai hayo yalisababisha  mgogoro wa kidiplomasia kati ya Kenya na Somalia na  kila nchi ikawaita nyumbani mabalozi wake .

 “ Tume imepata kwamba madai haya  mengine yakiwa lalama za muda mrefu hayana ushahidi wa kusababisha mgogoro wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili .  Ni kweli kwamba  Somlia ni nchi huru na maamuzi yake  yanachukuliwa kwa msingi huo’  sehemu moja ya ripoti hiyo imesema

" Hata hivyo kwa uangalizi wa karibu   madai hayo hayasaidii kwani nchi hizi mbili zina uhusiano wa karibu  kisiasa ,kiuchumi na kiutu’

 Ripoti hiyo imeongeza kwamba kutokana na mzozo huo wa kidiplomasia  watoto 3000 wa Somalia wanaosomea Kenya  hawakuweza kwenda shuleni  na pia mzozo huo ulivuruga oparesheni za wanajeshi wa Amisom ,kuvuruga biashara ya miraa na oparesheni za  kutoa misaada .