Uhamisho

Polisi 120 wa trafiki wahamishwa

Siku ya jumanne rais Uhuru Kenyatta alisema polisi sio adui wa raia na kuwahimiza wananchi kushirikiana nao ili kuhakikisha kwamba wakenya wote wako salama .

Muhtasari
  • Mageuzi hayo  yametangazwa kupitia arifa ya ndani iliyotolewa januari tarehe 27  ikiorodhesha wale walioathiriwa
  •  Polisi wa trafiki ndio hulaumiwa sana kwa maovu katika huduma ya polisi kwa  sababu ya kazi yao
Polisi wa trafiki

Zaidi ya maafisa  120 wa polisi wa trafiki wamehamaishwa katika mageuzi yanayolenga  kuboresha oparesheni za idara hiyo kote nchini .

 Maafisa waliohamishwa ni kutoka  Baringo, Uasin Gishu, Narok, West Pokot, Kericho, Nandi, Nakuru, Kajiado, Trans Nzoia, Laikipia na  Bomet

 Polisi hao walihamishwa kutekeleza majukumu ya kawaida  baada yaw engine kukumbwa na  visa vya ukosefu waidhamu na ukiukaji wa madili ya utendakazi katika idra ya trafiki . Mageuzi hayo  yametangazwa kupitia arifa ya ndani iliyotolewa januari tarehe 27  ikiorodhesha wale walioathiriwa

 Polisi wa trafiki ndio hulaumiwa sana kwa maovu katika huduma ya polisi kwa  sababu ya kazi yao . wakati  mwingine wao hujipata katika hali ngumu kwa kushambuliwa na wenye  magari wakishtumiwa kwa kuwa  wakali ama kuwaonea wenye magari kwa kuitish kiasi kikubwa cha faini kwa makosa madogo madogo .

 Siku ya jumanne rais Uhuru Kenyatta alisema polisi sio adui wa raia  na kuwahimiza wananchi kushirikiana nao ili kuhakikisha kwamba wakenya wote wako salama .

 Mageuzi hayo yamejiri siku chache tu baada ya makao makuu ya idara hiyo kuanya polisi dhidi ya kuweka vizuizi  kwenye barabara kuu nchini . vizuizi hivyo aghalabu vinatumiwa kama vituo vya kuwapunja fedha wenye magari  na hivyo inspekta mkuu wa polisi Hillary Mutyambai anataka vizuizi vya muda tu .