- Seneta Orengo hata hivyo amesema uamuzi hu unamaanisha kwamba mfumo wa sheria umevunjika na utovu wa madili umeingia katika idara ya mahakama .
- Rais wa chama cha wanasheria LSK Nelson Havi ametaka kuondolewa kwa jaji Patrick Otieno aliyetoa uamuzi huo kwa ukiukaji wa madili .
Agizo la mahakama linalomzuia naibu jaji mkuu kutohudumu kama jaji mkuu ni kitendo cha ugaidi wa idara ya mahakama amesema seneta wa Siaya James Orengo .
Mahakama kuu ya Meru siku ya ijumaa ilitoa maagizo ambayo ynamzuia Mwilu kuhudumu kama kaimu jaji mkuu na mwenyekiti wa tume ya JSC katika kesi inayotilia shaka hadhi yake .
Mlalamishi alidai kwamba Mwilu anakabiliwa na kesi ya ufisadi na itakuwa mapendeleo kumruhusu kuendelea kuhudumu kama mwanachama na rais wa mahakama ya juu Zaidi
Seneta Orengo hata hivyo amesema uamuzi hu unamaanisha kwamba mfumo wa sheria umevunjika na utovu wa madili umeingia katika idara ya mahakama .
Ukosoaji wa orengo kuhusu uamuzi huo sasa unashehei msururu wa maoni kama hayo na pingamizi kutoka kwa baadhi ya watu umetajwa kama njama ya baadhi ya watu kupunguza nguvu ya idara ya mahakama .
Rais wa chama cha wanasheria LSK Nelson Havi ametaka kuondolewa kwa jaji Patrick Otieno aliyetoa uamuzi huo kwa ukiukaji wa madili .