- Matiang’I amesema Nyache atapewa taadhima ya kupewa maziko ya kitaifa . Viongozi wakuu serikalini watahudhuria hafla ya mazishi ya Nyache katika uwaja wa Gusii .
- Mwili wa Simeon Nyachae uliwasili jana katika boma lake ,Nyosia Kisii .
Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiangi amesema usalama utaimarishwa wakati wa mazishi ya waziri wa zamani Simeon Nyachae anayezikwa leo jumatatu huko Kisii
Matiang'i amesema rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto ni miongoni mwa watakaohudhuria mazishi hayo .Aliyasema hayo siku ya jumapili alipzuru uwanja wa Gusii .
Matiang’I alikuwa ameandamana na gavana wa Kisii James Ongwa ,mwakilishi wa akina mama Janet Ongera ,katibu wa kudumu wa afya Susan Mochache na viongozi wengine kutoka eneo hilo kabla ya mazishi hayo baadaye leo .
Matiang’I amesema Nyache atapewa taadhima ya kupewa maziko ya kitaifa . Viongozi wakuu serikalini watahudhuria hafla ya mazishi ya Nyache katika uwaja wa Gusii .
" Tunataraji kumpa maziko ya utulivu na amai kiongozi huyo wetu .Kila kitu kiko tayari ,mahema yamewekwa ‘ Matiang’I aliwaambia wanahabari .
Alimtaja Nyachae kama kiongozi aliyependa Amani .
Sehemu ambako misa ya mazishi itafanyika imebadilishwa kutoka uwanja wa michezo wa Nyanturago hadi uwanja wa Gusii kwa sababu ya idadi kubwa ya wanaotarajiwa kuhudhuria .
Mwili wa Simeon Nyachae uliwasili jana katika boma lake ,Nyosia Kisii .