Kuwa tayari kwa uhaba wa maji jijini Nairobi siku mbili zijazo

Kampuni ya maji jijini Nairobi imewaagiza wakazi wa maeneo yatakayoathirika kuhifadhi maji ili wasitatizike

Muhtasari

•Maeneo yatakayoathirika ni pamoja na jiji nzima, maeneo yanaombatana na barabara ya Mombasa, Chuo Kikuu cha Nairobi, JKIA , Industrial Area na maeneo yanayoambatana na Jogoo road.

water vendors in Nairobi
water vendors in Nairobi
Image: The Star

Kampuni ya maji  ya Nairobi jijini Nairobi, (Nairobi City Water & Sewerage Company )imewapatia wakazi wa maeneo tofauti ya kaunti  ya Nairobi ilani ya kuwepo kwa ukame wa maji siku ya Alhamisi na Ijumaa.

Hii inatokana na utengenezaji wa barabara kuu ya kutoka JKIA  kuelekea Westlands ambao unaendelea .

Kupitia ujumbe wa umma, mkurugenzi mtendaji  wa kampuni hiyo , Nahashon Muguna ametangaza kuwa watakata mferenji wa maji ulio kwenye barabara kuu  ya Uhuru kuanzia thenashara asubuhi siku ya Alhamisi hadi asubuhi ya siku ya  Ijumaa.

 

“Hii itawezesha kubadilishwa kwa mifereji mzee inayoambatana na barabara kuu ya Uhuru kati ya eneo la Museum Hill na KBC ili kuonyesha wastani wa barabara kwa mkandarasi” Muguna alisema.

Maeneo yatakayoathirika ni pamoja na jiji nzima, maeneo yanaombatana na barabara ya Mombasa, Chuo Kikuu cha Nairobi, JKIA , Industrial Area na maeneo yanayoambatana na Jogoo road.

Wakazi wa maeneo hayo wameagizwa kuhifadhi maji ili wasitatizike katika kipindi hicho.