Muhtasari
•Rais Uhuru Kenyatta amesema kuwa serikali itawekeza shilingi bilioni 2.4 kwenye vita dhidi ya dhuluma ya kijinsia kufikia mwaka wa 2022. Kenyatta amesema kuwa kiwango hicho cha fedha kitaongezwa hadi bilioni 5.4 kufikia mwaka wa 2026 ili kuimarisha vita hiyo.
•Alisema kuwa bara Afrika limeshuhudia ongezeko ya shida hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja ambao umepita. Alitaja kuwa Kenya(50%), Liberia(50%), Central Afrika Republic(50%), Afrika Kusini(37%) na Cameroon(35%) ndiyo mataifa amabyao yamerekodi ongezeko kubwa zaidi ndani ya kipindi cha miezi 12 iliyopita.