•Kulingana na mchambuzi huyo ambaye anajihusisha sana na mrengo unaounga rais Kenyatta mkono, nyumba yake iliyo maeneo ya Runda iliteketea mida ya saa nane kasorobo usiku.
•Itumbi alikuwa ameandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter akiwaomba wazimamoto kukimbia na kusaidia kuzima moto ule.
Moto mkubwa uliteketeza nyumba ya mchambuzi wa siasa maarufu nchini, Mutahi Ngunyi usiku wa kuamkia Jumatano.
Kulingana na mchambuzi huyo ambaye anajihusisha sana na mrengo unaounga rais Kenyatta mkono, nyumba yake iliyo maeneo ya Runda iliteketea mida ya saa nane kasorobo usiku.
Hata hivyo hakusema kilichosababisha mkasa huo ulioharibu nyumba ambayo amemiliki kwa kipindi cha miaka 27.
Kabla ya Ngunyi kuthibitisha habari za mkasa huo, mwahabari na msemaji wa 'Hustler Nation' Dennis Itumbi alikuwa ametangaza mitandaoni kuhusu moto huo takriban dakika 16 baada ya kuibuka.
Itumbi alikuwa ameandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter akiwaomba wazimamoto kukimbia na kusaidia kuzima moto ule.
"Wazimamoto tafadhali fanyeni hara mkaokoe nyumba ya Mutahi Ngunyi iliyo Runda. NMS harakisheni mkasaidie jamaa ambaye anawaunga mkono. Natumai ako salama na familia yake pia iko sawa. Kando na ujumbe wangu, naweza omba tu usiende hasara kubwa na uwe salama." Itumbi aliandika kwenye mtandao wa Twitter
Dear Fire Brigade, please rush and save @MutahiNgunyi Runda House from FIRE. @NMS_Kenya quick action for a guy who supports you if nothing else. Hope the man is safe and family OK. Other than the tweet, I can only pray that you suffer the LEAST damage and be safe! pic.twitter.com/cqGmZSU6ic
— Dennis Itumbi, HSC (@OleItumbi) July 13, 2021
Ngunyi alionekana kutilia shaka jambo hilo kwani kulingana na yeye, moto huo uliibuka dakika 16 pekee kabla ya Itumbi kutangaza habari hizo na awali siku hiyo alikuwa amezungumzia swala la vurugu zilizojitokeza maeneo ya Kiambaa mwaka wa 2008 kwenye stesheni yake ya 5th Estate.
"Rafiki yangu Ole Itumbi, nyumba yangu iliyo Runda ya miaka 27 ilteketea 1.45AM. Uliambia Hustlers 2.01AM, takriban dakika 16 baadae. Hii ni baada yangu kuzungumzia vurugu zilizojitokeza Kiambaa mwaka wa 2008 kwenye runinga ya 5th Estate." Ngunyi aliandika.
My FREN @OleItumbi MY house in Runda for 27 years WENT on FIRE at 1.45 am. You TOLD the Hustlers at 2.01 am. About 16 minutes LATER. That is after I talked about KIAMBAA violence of 2008 on 5th Estate. Here is a BETTER picture than the one you POSTED. Enjoy. pic.twitter.com/w95WiY34H0
— Mutahi Ngunyi (@MutahiNgunyi) July 14, 2021
Hata hivyo, Itumbi alijibu kuwa ujumbe wa Ngunyi yalikuwa ya kitundu.