Shule ya Sigalame yateketea kwa mara ya tano

Chanzo cha moto huo bado hakijabainika lakini polisi wanashuku kuwa moto huo ulianzishwa na mtu makusudi.

Muhtasari

• Hakuna jeraha lililoripotiwa katika moto wa jana usiku lakini wanafunzi wengi walipoteza mali zao.

• Shule hiyo ilifungwa mwezi uliopita baada ya moto kuteketeza bweni moja. Polisi wanaamini kuwa moto huo umewashwa kwa makusudi na wanataka kuwapata walio nyuma yake.

• Chanzo cha moto huo bado hakijabainika lakini polisi wanashuku kuwa moto huo ulianzishwa na mtu makusudi.

Image: TWITTER.COM/SIGALAMEALUMNI/STATUS

Polisi wamepiga kambi katika Shule ya Upili ya Sigalame eneo la Funyula, Kaunti ya Busia baada ya moto kuteketeza mabweni mawili katika shule hiyo jana usiku.

Chanzo cha moto huo bado hakijabainika lakini polisi wanashuku kuwa moto huo ulianzishwa na mtu makusudi. Hiki ni kisa cha tano cha moto kutokea katika shule hiyo ambayo ilikuwa tu imefunguliwa tena.

Shule hiyo ilifungwa mwezi uliopita baada ya moto kuteketeza bweni moja. Polisi wanaamini kuwa moto huo umewashwa kwa makusudi na wanataka kuwapata walio nyuma yake.

Hakuna jeraha lililoripotiwa katika moto wa jana usiku lakini wanafunzi wengi walipoteza mali zao.

Polisi wanasema wameelezea hofu kutokana na ongezeko la visa vya moto shuleni nchini na wanataka wakuu wa shule kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo. Angalau shule tano zimeteketezwa katika visa tofauti katika wiki zilizopita pekee.

Kwingineko,

Mshukiwa mmoja wa ujambazi aliuawa kwa kupigwa risasi Jumanne usiku baada ya yeye na wenzake wanne kuvamia mtaa mmoja karibu na eneo la Mlango Kubwa, Mathare na kuanza kuwaibia wakazi.

Genge hilo pia lilikuwa limewafunga walinzi waliokuwa zamu na kumpokonya simu yake ya rununu kabla ya kuendelea na shuguli zao.

Polisi walipewa taarifa na kufanikiwa kufika na mmoja akwauawa katika msako uliyofuatia. Wenzake walifanikiwa kutoroka. Polisi wanasema visa vya wizi kutumia silaha vimeongezeka tangu kuondolewa kwa amri ya kutotoka nje wiki iliyopita.