Amnesty International yaomba Kenya kutowalazimisha watu kuchomwa chanjo ya Corona

Muhtasari

• Shirika la kutetea haki za binadamu Amnesty International tawi la Kenya limetoa wito kwa serikali ya Kenya kutowalazimisha raia wake kupewa chanjo ya Covod -19.

• Siku ya Jumapili Waziri wa afya wa Kenya Mutahi Kagwe alisema watu ambao hawajachanjwa watazuiwa kupata huduma za usafiri wa umma, ndege na treni.

MAJARIBIO YA CHANJO: Chanjo mpya ya Pfizer na BioNTech ina kinga ya asilimia 90 Picha: REUTERS
MAJARIBIO YA CHANJO: Chanjo mpya ya Pfizer na BioNTech ina kinga ya asilimia 90 Picha: REUTERS

Shirika la kutetea haki za binadamu Amnesty International tawi la Kenya limetoa wito kwa serikali ya Kenya kutowalazimisha raia wake kupewa chanjo ya Covod -19.

Katika taarifa shirika hilo lilsema: 'Kamati ya kitaifa ya kukabiliana na janga la Corona iharakishe programu za elimu zinazofaa ili kushughulikia chanjo kwa uwazi na kushughulikia taarifa potofu'.

''Ingawa kuna sababu halali za afya ya umma kwa watu wengi iwezekanavyo kupata chanjo, sababu hizi zisiwanyime watu haki ya kufanya kazi, kupata huduma muhimu zikiwemo elimu, afya na usalama pamoja na uhuru wao wa kutembea. Haya yote ni haki za kimsingi na uhuru wa kikatiba,'' ilisema taarifa hiyo.

Siku ya Jumapili Waziri wa afya wa Kenya Mutahi Kagwe alisema watu ambao hawajachanjwa watazuiwa kupata huduma za usafiri wa umma, ndege na treni.

Utaratibu huo utaanza kufanya kazi Disemba 21.

Kenya imepanga kuchanja watu milioni 10 mpaka kufikia mwishoni mwa Disemba mwaka huu .

Mpaka sasa ni chini ya asilimia 10% ya watu wamepatiwa chanjo.