Mwanamuziki wa Rhumba Defao afariki dunia

Muhtasari

•Le General  ni mwanamuziki mwenye aliyekuwa na kipaji cha kutunga na kuimba nyimbo kwa sauti nyororo na yakuvutia kwa wapenzi wa Rhumba.

Msanii wa muziki wa Kongo Lulendo Matumona, anayejulikana zaidi kwa jina la Jenerali Defao alikufa Jumatatu, Desemba 27, 2021, huko Douala, Kamerun.
Msanii wa muziki wa Kongo Lulendo Matumona, anayejulikana zaidi kwa jina la Jenerali Defao alikufa Jumatatu, Desemba 27, 2021, huko Douala, Kamerun.
Image: Picha: ZOOM-ECO.NET

Mwanamuziki nguli wa nyimbo  za Rhumba kutoka Congo, Le General  Defao Matumona amefariki dunia   nchini Cameroon .

Defao ambaye alikuwa na umri wa takriban miaka 62 amefariki  dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi. Kifo chake kimejiri wakati akiwa ziarani ya kuwatumbuiza mashabiki wake nchi ya Cameroon.

Mwanamuziki huyo alizaliwa Disemba 03, 1958, Kinshasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia  ya Congo.

Le General  ni mwanamuziki aliyekuwa na kipaji cha kutunga na kuimba nyimbo kwa sauti nyororo na yakuvutia kwa wapenzi wa Rhumba. Alijizolea umaarufu mkubwa kwa miondoko yake ya Ndobolo.

Aliweza kutambulika rasmi kwenye tasnia ya muziki wa Rhumba mnamo mwaka wa 1976, wakati alitoa nyimbo kubwa kama School of love, Kikuta family na Sidewalk

Wanamuziki Fally Ipupa na Ferre Gola walikuwa miongono mwa wa kwanza kuwasilisha ujumbe wao wa rambirambi, wakieleza kifo chake kuwa ni hasara kwa Afrika