Polisi awaua wenzake wawili kisha kujipiga risasi katika kituo cha polisi cha Moyale

Kumber alichukua jiwe na kumpiga Konstebo Noah Odero kichwani kabla ya kuchukua bunduki yake.

Muhtasari

•Kumber alitembea hadi kwenye hifadhi ya silaha ya kituo ambako alikutana na afisa mkuu koplo Francis Kokwe na kumuua papo hapo.

•Mwili wake uligunduliwa ndani ya nyumba muda mrefu baada ya tukio hilo kutokea.

Bunduki
Bunduki
Image: Andrew Kasuku
Bunduki
Bunduki
Image: Andrew Kasuku

Afisa mmoja anayehudumu katika kituo cha polisi cha Moyale mjini Marsabit amewaua wenzake wawili na kuwajeruhi wengine kabla ya kujiua.

Wenzake walisema alitakiwa kufika kazini.

Walioshuhudia walisema konstebo Lawrence Kumber alikutana na mwenzake ambaye alikuwa akitoka kazini na kuelekea nyumbani kwake ndani ya kituo hicho ili kuchukua stakabdhi fulani kabla ya kurudisha bunduki yake aina ya AK47.

Kumber alichukua jiwe na kumpiga Konstebo Noah Odero kichwani kabla ya kuchukua bunduki yake.

Kisha alitembea hadi kwenye hifadhi ya silaha ya kituo ambako alikutana na afisa mkuu koplo Francis Kokwe na kumuua papo hapo.

Kisha akamgeuzia bunduki askari mwingine aliyejulikana kwa jina la Ezekiel Matete na kumuua kwenye lango la ghala la kuhifadhia silaha.

Kumber pia alimpiga risasi na kumjeruhi afisa wa tatu begani huku wengine wakijificha.

Kisha alitoroka kutoka kwenye ghala la silaha hadi nyumbani kwake ambako alijipiga risasi.

Mwili wake uligunduliwa ndani ya nyumba muda mrefu baada ya tukio hilo kutokea.

Bunduki ililala karibu na mwili.

Maafisa wawili waliojeruhiwa walikimbizwa hospitalini ambapo walilazwa katika hali shwari huku miili ikihamishiwa katika hifadhi ya maiti ya kaunti ndogo ya eneo hilo.

Mkuu wa polisi wa eneo la Mashariki Rono Bunei alisema bado hawajabaini nia ya tukio hilo.

"Silaha na vielelezo vingine vimekusanywa tunapochunguza tukio hili la kusikitisha," alisema.

Alisema kuwa wiki iliyopita afisa huyo alikuwa amefunguwa miongoni mwa wale watakaopewa bunduki kutoka kwa ghala la silaha, kwa sababu ya tabia yake.

Kwingineko, afisa wa polisi aliuawa Jumamosi usiku katika ajali iliyotokea kwenye barabara ya Nothern Bypass jijini Nairobi.

Konstebo Boniface Mugunda aliyekuwa akihudumu katika makao makuu ya DCI alikuwa akiendesha pikipiki yake alipogongwa na dereva asiyejulikana.

Bastola yake aina ya Ceska na vitu vingine vya thamani vilipatikana.

Polisi walisema alitangazwa kuwa amefariki alipofika katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Kenyatta. Uchunguzi umeanzishwa.

Hakuwa na majeraha ya mwili na alikuwa na vifaa vyake vya kujikinga wakati wa ajali.