logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua avunja kimya kuhusu bei ya juu ya mafuta

“Humtaji mwajiri wako kwa kiburi. Fanya hivyo kwa unyenyekevu na adabu,” Gachagua alishauri.

image

Habari17 September 2023 - 12:26

Muhtasari


  • Alieleza kuwa ni fursa nzuri kuwahudumia Wakenya na kwa hivyo, viongozi hawafai kuwa wazembe na kuwadharau watu.
Naibu Rais Rigathi Gachagua akiwa KICC alipoongoza nchi kuadhimisha Siku ya Ushirika,

Naibu Rais Gachagua Jumapili alivunja kimya chake kuhusiana na ongezeko la bei ya mafuta iliyotangazwa na Mamlaka ya Kudhibiti Kawi na Petroli (EPRA).

Gachagua, akitoa kauli yake ya kwanza baada ya kuwasili nchini kutoka kwa safari ya kikazi nchini Colombia, alieleza kuwa kupanda kwa bei ya mafuta ni suala la kimataifa na kuwataka Wakenya kuwa na subira huku serikali ikijitahidi kutatua suala hilo.

“Kwa heshima kubwa, ningependa kuwasihi watu wa Kenya kufahamu kwamba suala la bei ya mafuta ni changamoto duniani kote. Mambo yatakuwa mazuri tunapoendelea," DP alisema.

Alieleza kuwa serikali inafahamu na inajali changamoto zinazowakabili Wakenya kutokana na gharama ya juu ya maisha.

"Rais William Ruto anaendelea kujitolea kutafuta suluhu za kudumu na endelevu kwa changamoto za kiuchumi zinazokabili taifa letu kuu," aliahidi.

Aliendelea kuwakemea Makatibu wa Baraza la Mawaziri na washauri ambao wameshutumiwa kwa kutojali changamoto zinazowakabili Wakenya.

Naibu Waziri wa Biashara, Moses Kuria na mshauri wa masuala ya kiuchumi wa Rais William Ruto David Ndii, alibainisha kuwa maoni yao yalikuwa ya kizembe na hayawakilishi wadhifa rasmi wa serikali au wa Rais William Ruto.

Gachagua alifichua kuwa hata alipokuwa nje ya nchi, alikuwa akifuatilia kesi na kutilia shaka busara katika njia ambayo viongozi hao wawili wamechukua kushughulikia suala hilo nyeti.

Alieleza kuwa ni fursa nzuri kuwahudumia Wakenya na kwa hivyo, viongozi hawafai kuwa wazembe na kuwadharau watu.

“Humtaji mwajiri wako kwa kiburi. Fanya hivyo kwa unyenyekevu na adabu,” Gachagua alishauri.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved