logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya yakana madai ya kuuza uwanja wa ndege wa JKIA

Kuna mipango ya kubadilisha uwanja wa ndege kuwa wa kisasa na kujenga eneo jipya la mapokezi.

image
na Davis Ojiambo

Habari23 July 2024 - 12:35

Muhtasari


  • • Seneta wa Kisii Richard Onyoka alidai kupata fununu kuhusu uuzaji wa uwanja huo.
  • • Madai ya kuuzwa kwa uwanja wa JKIA zimechochea maandamano ya kupinga serikali Jumanne hadi JKIA.

Serikali imepuuzilia mbali madai kuwa kuna njama ya kuuza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) kwa wawekezaji wa kigeni.

Ripoti kuhusu madai ya kuuzwa kwa uwanja huo wa ndege zimetawala mitandao ya habari nchini Kenya na kusababisha maandamano ya Jumanne yaliyopewa jina la 'OccupyJKIA'.

Mkuu wa mawaziri ambaye pia ni kaimu waziri wa uchukuzi Musalia aliambia Kamati ya Bunge ya Kitaifa ya Bajeti kwamba uuzaji wa Uwanja huo unaweza tu kufanywa kupitia idhinisho la bunge.

“Uwanja wa ndege hauuzwi. Hii ni mali ya umma, rasilimali muhimu. Ikiwa ungeuzwa, lazima mchakato kamili wa umma ambao bunge limeidhinisha uzingatiwe,” Mudavadi aliwaambia wabunge.

Alisema kuna mipango ya kubadilisha uwanja wa ndege kuwa wa kisasa na kujenga eneo jipya la mapokezi.

Seneta wa Kisii Richard Onyoka alidai kupata fununu kuhusu uuzaji wa uwanja huo. Anadai serikali imeafikia uamuzi kukabidhi umiliki wa JKIA kwa mwekezaji wa kigeni.

Ripoti za madai ya kuuzwa kwa uwanja huo wa ndege zimechochea maandamano ya kupinga serikali Jumanne hadi JKIA.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved