logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ndindi Nyoro apokea shutuma kutoka kwa Wabunge sababu ya matumizi mabaya ya afisi

Mbunge wa Kiharu mheshimiwa Ndindi Nyoro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya bajeti katika bunge la taifa .

image
na Evans Omoto

Yanayojiri12 March 2025 - 08:37

Muhtasari


  • Ndindi Nyoro ni msomi aliyefuzu kwa cheti cha shahada ya Uchumi kutoka chuo kikuu cha Kenyatta na kwa muda uliopita alirodheshwa na mashirika mbalimbali ya utafiti kama kiongozi mpevu na mchapa kazi.
  • Katika sherehe za Hamsini na tisa( 59) za kusherehekea siku ya Jamhuri Rais William Ruto aliwahi kumtuza kama kiongozi mpachapazi kwa kuendeleza maendeleo katika eneobunge lake la Kiharu.

Mbunge wa Kiharu mheshimiwa Ndindi Nyoro ambaye ni mwenyekiti wa  kamati ya bajeti katika bunge la taifa .

Ndindi Nyoro ni msomi aliyefuzu kwa shahada ya Uchumi kutoka chuo kikuu cha Kenyatta na kwa muda uliopita alirodheshwa na mashirika mbalimbali ya utafiti kama kiongozi mpevu na mchapa kazi.

Katika sherehe za Hamsini na tisa( 59) za kusherehekea siku ya Jamhuri Rais William Ruto aliwahi kumtuza kama kiongozi mpachapazi kwa kuendeleza maendeleo katika eneobunge lake la Kiharu.

Nyoro alikuwa akishikilia nafasi ya uenyekiti wa bajeti katika bunge la taifa tangu serikali ya Kenya Kwanza ilipochukua hatamu za uongozi na amekuwa kipenzi cha wengi kwa kuonyesha uzingativu wa hali ya juu kazini.

Kwa siku chache zilizopita bwana Nyoro amekuwa kimya tofauti na alivyokuwa mtetezi sugu wa bwana Ruto,hata inakumbukwa wengi walisawiri ushirikiano wa Rais Ruto na  Nyoro kama ulikuwa ni mwiba hatari kwa aliyekuwa naibu wa Rais enzi hizo Rigathi Gachagua.

Kulingana na mawimbi ya mageuzi mbalimbali yaliyotendeka katika kamati za bunge yaliyomlenga mwenyekiti wa kamati  ya bajeti bwana Nyoro na kuweza kumwondoa ili nafasi yake ijazwe na mwenyekiti mwingine.

Katika hoja zilizotolewa na wabunge mbalimbali ili kuweza kujadili na kupiga msasa utendakazi wa bwana Nyoro katika kamati yake ya bajeti kama mwenyekiti viongozi mbalimbali waliweza kumkashifu kwa matumizi mabaya ya afisi.

Kiuongozi wa waliowengi bungeni pia ambaye ni mbunge wa Kikuyu bwana Kimani Ichungwa aliweza kumkashifu bwana Nyoro kwa kujilimbikizia Madaraka tele kwa kutenga bajeti ambayo haioani na bajeti ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya maeobunge yote wakilishi katika bunge la  Taifa.

Vilevile Kiongozi wa walio wachache katika Bunge la Taifa Junnet Mohammed aliweza pia kumshutumu mwana Nyoro kwa kuwa mbinafsi na mwenye kujijali alipojitengenezea bajeti ya hela nyingi kwa ajili ya eneo bunge lake katika kile ambacho kilitajwa kama kutokuwa na usawa kwa kutekeleza wajibu wake ipasavyo kama mwenyekiti wa bajeti.

Kulingana na mujibu wa bwana Ichunhwa na Junet eneobunge la Kiharu lilipokea mgao wa fedha nyingi za bajeti na za kimaendeleo kushinda maeneobunge yoyote 289 kuashiria upendeleo na ukiukaji mkubwa wa Katiba.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved