Mkusanyiko wa Habari na Matukio Muhimu Tarehe 24 Juni 2019
Jaza fomu za kodi kabla ya makataa
Una siku sita zilizosalia ili ujaze fomu za kuthibitisha kwamba umelipa kodi mwaka uliopita . wale wasio na mapato wanatakiwa kujaza fomu hizo kuonyesha kwamba hawakulipa kodi chochot kama kodi .
Jaji Mkuu kuunda jopo la kusikiza kesi za kupinga marupurupu ya wabunge
Kesi mbili zinazolenga kuwazuia wabunge kupokea marupurupu ya nyumba zimehamishwa hadi kwa jaji mkuu ili aunde jopo la majaji wa kuzisikiliza . mwanaharakati Okiya Omtatah na tume ya SRC wanataka wabunge kuzuiwa kupokea shilingi elfu 250 kila mmoja kama marupurupu ya nyumba na kurejesha fedha walizopewa .
Watahiniwa wa KCPE kuchagua shule wanazotka kujiunga nazo
Watahiniwa wanaofanya mtihani wa KCPE mwaka huu wana hadi mwisho wa mwezi ujao kutathmini upya shule za upili wanazotaka kujiunga nazo mwezi januari . mtindo huo ni mpya kwani kwa kawaida watahiniwa huzichagua shule za upili baada ya matokeo kutolewa . katibu wa kudumu wa elimu Belio Kipsang amesema hatua hiyo itapunguza muda unaotumiwa katika utaratibu wa usajili wa kidato cha kwanza .
Zoezi la kuwaajiri majaji laingia wiki ya pili
Shughuli ya kuwaajiri majaji wa mahakama ya rufaa imeingia wiki ya pili leo huku watu wanne wakitarajiwa kuhojiwa leo .wanne hao ni majaji Hedwig Ong’udi, Hellen Omondi, Joseph Sergon na Nixon Sifuna. Jopo linaloongozwa na Jaji mkuu David Maraga linatarajiwa kuwahoji watu 33 waliotuma maombi ya kupewa kazi hizo kufikia julai tarehe mosi .
Ugonjwa wa kipindupindu unaweza kutibiwa
Wagonjwa walio na daalili za ugonjwa kipindupindu wanaweza kupona endapo watatipiwa mara moja . mtaalm wa afya ya umma Josephine Odanga amesema mgonjwa wa kipindu pindu anafaa kukimbizwa kwa kituo cha matibabu haraka iwezekanavyo ili kuongezwa maji mwilini .