HATARI:Yafahamu makundi ya kigaidi yanayouhangaisha ulimwengu

  Ugaidi ni zimwi ambalo sasa  ni  tatizo la ulimwengu mzima na  matiafa mengi sasa ymegundua kwamba yanahitaji juhudi za pamoja na ushirikiano ili kuyaangamiza makundi hayo .  Kati ya vifo vya  watu 18,814  kote duniani ,zaidi ya nusu ya vifo hivyo viulisababishwa na makundi manne makuu ya kigaidi ambayo ni Islamic State, Taliban, Al-Shabaab  na  Boko Haram. Shughuli za maundi hayo zimeyafnya maeneo yanakohudumu kama vile  Afghanistan , Iraq,Nigeria ,Somalia na Syria kutajwa kama nchi hatari zaidi . haya hapa maelezo ya mukhtasari kuhusu baadhi ya makundi hatari zaidi ulimwenguni .

Islamic State

Kundi hili ambalo pia hujulikana kwa kiarabu kama Daesh au  majina ya ufupisho ya ISIS  na ISIL, lilikuwa hatari zaidi katika miaka mitatu iliyopita kabla ya kupunguzwa makali na juhudi za pamoja za Marekani na washirika wake na makundi mbali mbali ya wapiganaji wanaovisaidia vikosi vya usalama vinavyopambana na ugaidi katika mataifa ya Iraq na  Syria . Kundi hilo liliyaenga pia mataifa yalio mbali na mashariki ya kati kama vile barani uropa na Asia .

Mashambulzi mengi ya ISIL yalikuwa ya mabomu .pia kundi hilo lilishiriki utekaji nyara wa watu na mauaji ya kuwakata watu shingo. Kwa sasa hata hivyo makali yake yamedidimia baada ya kuuawa kwa kiongozi wake wa kwanza Al baghadadi .

Taliban

Kundi hilo lenye  chimbuko lake  nchini Afghanistan  limekuwa katika vita na majeshi ya muungano yanayoongozw ana marekani tangia mwaka wa 2001  na limesalia na nguvu za kusababisha maafa katika sehemu nyingi za mashariki ya kati . kudikia  katikati ya mwaka wa 2017 kundi hilo lilikuwa likithibiti asilimia 11 ya sehemu ya ardhi ya Afghanistan na lilikuwa likilumbaia asilimia 29 ya wilaya 398 za taifa hilo .  Kundi la Taliban linendelea na oparesheni zake katika asilimia 70 ya mikoa ya Afghanistan .

 Al-Shabaab

Kundi hilo la kigaidi lilichipuka mwaka wa 2006 . Limejitambua kama sehemu ya mtandao wa kigaidi wa al qaida  na linahudumu nchini Somalia lakini pia limefanya mashambulizi ya kila mara katika mataifa ya  Ethiopia, Kenya  na Uganda. Al shabaab lilikuwa kundi hatari zaidi Kusini mwa Jangwa la Sahara  mwaka wa 2017.Thuluthi mbili ya vifo vilivyosababishwa na mshambulizi ya al shabaab vimetokea katika mji mkuu wa Soalia ,Mogadishu . kisa kibaya zaidi kilitokea mwaka wa 2017 oktoba wakati watu 588 walipouawa na wengin zaidi ya 316 kujeruhiwa .

Boko Haram

Kundi hilo lenye makao yake nchini  Nigeria  pia linafahamika  kwa jina lake la kiarabu (Jama’tu Ahlis Sunna Lidda’awati wal-Jihad)  na wakati mmoja lilikuwa hatari zaidi duniani  lakini uwezo wake umekuwa ukididimia tangu mwaka wa 2014  na hivi maajuzi limegawanyika katika makundi madogo madogo  . Tangu lilipochipuka  kaskazini mashariki mwa nchi hiyo  mwaka wa 2002  , Boko  haram  pia limesambaa hadi katika mataifa ya Chad, Cameroon  na  Niger na limesema linaunga mkono kundi la Islamic State . Mashambulizi mengi ya kundi hilo yalitekelezwa  nchini Nigeria katika Jimbo la Borno  ,huku visa vichache vidogo vikitekelezwa katika nchi jirani za Cameroun na Niger .Kundi hilo limelaumiwa kwa visa vingi vya utekaji nyara watu na kutekeleza mashambulizi ya kujitoa mhanga .

Makundi mengine ya kigaidi

  Kando na makundi haya  manne ya kigaidi kuna mashambulizi mengi ambayo hutekelezwa na vikundi  mbali mbali likiwemo kundi la al qaeda.Mwaka wa 2019 makundi 169  yalihusika na takriban kifo kimoja  lakini ni makundi 130 yaliyotekeleza mashambulizi hayo. Mengi ya makundi haya ni madogo lakini makubwa kama vile al qauda yana wapiganaji takriban elfu 30 katika  mataifa 17 ya mashariki ya kati na afrika. Nchini Syria kuna makundi kadhaa yakiwemo  Hayat al-Tahrir al-Sham (Awali yaliyojulikana kama Jabhat Fateh al-Sham na  Al-Nusra)  na Jaysh al-Islam. Nchini Pakistan  makundi  yaliyotambulika kwa kusababisha maafa   kupitia mashambulizi   ni pamoja na Lashkar-e-Jhangvi  na the Khorasan Chapter  linalohusiana na  Islamic state . Katika taifa jirani la India  kundi hatari zaidi ni la chama cha kikomunisti (Maoist) kwa jina jingine Naxals,  ambalo lilisababisha vifo 205 kupitia mashambulizi 190. Mwaka jana makundi matano tofauti  yakiwemo Lashkar-e-Taliba, Jaish-e-Mohammad na Hizbul Mujahideen, yalisababisha vifo vya watu 102. Thamani ya mali iliyoharibiwa kwa sababu ya vitendo vya kigaidi mwaka wa  2017 pekee ilikuwa dola bilioni 52.