hii hapa orodha ya baadhi ya wanasiasa wa kike walio na mitindo ya mavazi ya kuvutia .
Esther Passaris( umri ,miaka 54)
Passaris ambaye ni mfanyibiashara ,mhisani na mwanasiasa ni mrembo wa kuchachawiza . mavazi yake na miondoo pia haijanyima chochote na wakati wote akiwa amejikwatua kuvutia . Pia amefahamu jinsi ya kila mara kuonekana chipukizi na kamwe umri haujamasaliti.
Anne Waiguru( Miaka 52)
Gavana huyu wa Kirinyaga wakati wote anapendeza kwa ajili ya mavazi yake bomba . Rangi nyekundu bila shaka ndio chaguo lake .
Susan Kihika( miaka 45 )
wakili huyu ambaye ni seneta wa nakuru wakato wote anavutia kwa ajili mkwatuo wake wa kupendeza . mtindo wake hauhitaji kumtoa jasho ili kuonekana kama ua .
Wavinya Ndeti( Miaka 51 )
mwanasiasa huyu wakati wote anabubujikwa usasa na anavutia katika muonekano . ni mojawapo ya wanasiasa wa kike wenye miondoko ya kisasa .
Millicent Omanga
Seneta huyo chipukizi ana mvuto wa umbo ambalo wengi huzuzulika nalo- na amefahamu makali ya umbo hilo hivyo basi mavazi yake huingiana vyema sana na mwili wake .
Sonia Birdi
mwanamke wa kwanza mwenye asili ya kiasia kuhudumu katika bunge la taifa . Urembo wake wa kiasili na bayana na bila hajafelisha kupitia mavazi na mtindo wake . wakati wote ana muondoko ya hadhi na wa kipekee .