“ BBI iliyoanzishwa na rais Kenyatta ilifaa kuwahusisha wakenya wote . ni jambo la kusikitisha kwamba sasa wanasiasa wameutakanyara utaratibu mzima na kusababisha mgawanyiko hata zaidi’ Duale amesema .Duale, ambaye hajahudhuria mkutano wowote wa BBI ameshikilia kwamba hana mpango wa kuhudhuria mkutano wowote wa BBI isipokuwa inayohudhuriwa na naibu wa rais William Ruto na rais Uhuru Kenyatta.
“ kwa sasa nimejawa na majukumu ya bunge linalorejelea vikao vyake wiki ijayo .watu wa kaskazini mashariki mwa nchi wana matatizo mengi kama vile ukosefu wa usalama ,kufungwa kwa shule na suala la sensa .Haya ndio masuala ninayoyazingatia kwa sasa ‘ amesema Duale . Matamshi ya Duale yanajiri siku moja siku mbili tu baada ya rais Uhuru Kenyatta kusema kwamba mikutano ya BBI inayoendelea katika sehemu mbali mbali za nchi hailengi kumtenga yeyote .