Gavana wa Murang’a Mwangi wa Iria amefutilia mbali leseni za wamiliki wa mabaa waliokaidi agizo la kuyafunga maeneo hayo ya burudani kama ilivyoagizwa na kundi la kushughulikia dhrura katika kaunti hiyo .
Siku ya jumatatu gavana huyo na kamishna wa kaunti Mohamed Barre walisema mrundiko wa watu na hali mbaya ya usafi huenda ikalazimu kufungwa kwa baadhi ya baa .waliwashauri wakaazi kuburudi kwa kwa vinywaji vyao wakiwa nyumbani .
Wawili hao walisema watu walevi hawataweza kujikinga dhidi ya virusi vya corona .Kufikia jumanne gavana wa Iria alisema leseni za baa hio zimefutiliwa mbali baada ya wenyewe kukosa kuafikia mahitaji yaliyotolewa kama mojawapo ya njia za kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona .