Hofu:Wahudumu wa afya sasa wapo katika hatari ya juu ya kuambukizwa virusi vya corona

Kagwe
Kagwe
Wahudumu wa afya wameanza kulipia gharama ya juu katika janga la corona kwa kupoteza maisha yao ili kuokoa maisha ya wengi  kwa sababu ya hatari waliomo ya kuambukizwa virusi hivyo.

Kila siku wanayoripoti kazini kuwahudumia wagonjwa ni hatua moja wanayojitia karibu na uwezekano wa kuambukizwa  ugonjwa huo. Ripoti zaarifu kwamba  wahuduu wa afya, maafisa wa kliniki na  wauguzi wameambukizwa ugonjwa huo na hata wengine wameaga dunia.

Kifo cha wiki jana cha daktari  Doreen Lugaliki  ni ishara tosha kwamba wahudumu hao wa afya  wapo katika hatari zaidi kuliko kitengo chochote cha wapambanaji dhidi ya janga la corona.

Serikali na wadau wengine wamejaribu kuwapa hakikisho la usalama wao wa kutoa vifaa kama vile PPE  lakini misaada hiyo haijatosha jambo ambalo linazidi kuhatarisha maisha ya wahudumu wengi.

Licha ya hatari hiyo wahudumu wengi wa afya wamejitolea muhanga kuendelea na kazi zao na mengi yanafaa kufanywa ili kuwalinda kwani wao pia wana familia na wapendwa wao watakaoathirika sana endapo  wataangamia katika janga hili la corona.