Huenda Mitihani ya KCPE na KCSE ikafanywa mwaka ujao

Watahiniwa wa  KCPE  na  KCSE  huenda wakaifanya mitihani hiyo ya kitaifa Aprili mwaka ujao ,waziri wa elimu George Magoha amesema .

Magoha amesema  Aprili ndio  muda wa mwisho ambao mitihani hiyo inaweza kufanywa  iwapo shule zitafunguliwa mwezi septemba kama ilivyoagizwa na rais Uhuru Kenyatta .

" kuhusu kalenda ya shule ,serikali inafaa kuzingatia  muda wa mwisho ambao  shule zinavyoweza kufunguliwa na watahiniwa kuifanya mitihani’ amesema Magoha

Magoha amesema majadiliano yanaendelea  miongoni mwa wadau na katika wiki mbili zijazo ,itafahamika bayana endapo shule zitafunguliwa septemba ili watahiniwa waweze kuifanya mitihani hiyo kufikia Aprili mwaka ujao

Magoha  ameyasema hayo alipofika mbele ya kamati inayoshughulikia  hali ya Covid 19 nchini . Kamati hiyo  inayoongozwa na seneta wa Nairobi  Johnson Sakaja.