Ilikuaje: Alice asimulia changamoto alizopitia baada ya kukeketwa

alicemasinteradiojambo
alicemasinteradiojambo
Alice Kamande, 28, ni mama ambaye alipitia katika njia ya ukeketaji pia ni nusura.

Alisema kuwa alikeketwa akiwa na umri wa,12, na katika ukeketezaji, wazazi wa kike ndio huwapeleka wasichana wao kukeketwa.

"Mama ndio alinipeleka kukeketwa nukiwa na umri wa 12 mwaka wa2006,"Alieleza Alice.

Pia aliweza kueleza kuwa baada ya ukeketezaji msichana hupitia changamoto nyingi kama uvaji wa damu hadi mtu kufa, unasikia uchungu ukienda kukojoa, na kutopewa dawa na pia aliweza kuadhiriwa kimawazo.

"Nikizaa pia niliweza kupitia changamoto kwa maana kidonda hicho cha ukeketezaji ni cha milele na kimefunga njia ya mtoto ya kupitia,"Aliongea Alice.

Alice alisema kuwa utekeketezaji wa wasichani katika jamii yao wanasema huwa inazuia kupata mimba za mapema, kutokuwa na haja na wanaume pia ni tamaduni za jamii ya ambazo babu walikuwa wanafanya kwa hivyo wamefuata tamaduni.

Katika ukeketajih uwa wanatumia visu na wembe, na unaweza kupatwa na magonjwa mbalimbali.

"Huwa wanatumia visu au wembe na ni kisu kimoja tu kitakachokeketeza wasichana zaidi ya 10, hapo unapata wengi wanapatwa na magonjwa mbalimbali,

"Pia wakati huo wa ukeketezaji wazazi wa wanawake huwa wanakuzuia ili kuhakikisha kuwa umekeketezwa ipasavyo,"Alice alisema.

Alisema kuwa ukikeketwa inachukua muda wa mwezi mmoja ili msichana aweze kupona, dawa yao ambayo huwa wanatumia ni kinyesi cha ng'ombe.

Baada ya Alice kupitia hayo yote hakulaza damu bali waliweza kuunda kikundi cha kuwaelimisha wasichana madhara ya ukeketezaji.

"Si kukaa chini baada ya kupitia hayo bali tulianzisha kikundi ambacho kinaitwa (Naretondoi ) ambacho kinamaanisha Empowering girl child,

"Nilisimama ili kuwaelimisha wasichana na ndugu zangu madhara ya ukeketezaji na wasipitie uchungu ambao niliweza kupitia,"Alizungumza Kamande.

Aliweza kuandamana na mwenyekiti wa youth advocate,.

Matilda aliweza kusema kuwa changamoto ambazo wanapitia kama kikundi ni kuwa jamii haijakubali mabadiliko.

Pia wanajamii wamezoeshwa pesa kwa hivyo ukienda kuweka mkutano kama haujawalipia nauli na kuwapa kitu kidogo hawawezi kuenda katika mkutano wao.

"Nilisimama kama mwenyekiti wa youth Advocate baada ya kesi ya msichana ambaye alikeketwa sehemu za Meru na kufariki baada ya kuvuja damu,"

"Nilijiuliza kama huyu ni kijana mwenzetu alikeketwa na kufariki, hakuna haja ya kukaa kimya ilhali sisi wenyewe ndio tunaumia ,ndio maana tulianza kampeni ya wasichana wasikeketwe,"Alieleza Matilda.

Matilda alisema kuwa atakaye patikana akimdhulumu au kumkeketa msichana ata fungwa kifungo kisicho pungua miaka mitatu au alipe mahakama dhamana ya shillingi 200,000.