Je atawakwamua? Mikel Arteta ateuliwa rasmi kama kocha wa Arsenal

arteta
arteta

Arsenal imemteua kiungo wake wa zamani Mikel Arteta kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo.

Kocha huyo mwenye miaka 37 ameshinda kombe la FA mara mbili akiwa na kikosi cha Gunners katika misimu mitano aliyokipiga na vigogo hao wa London.

Anachukua nafasi ya Mhispania mwenzake, Unai Emery ambaye alitimuliwa mwezi Novemba kutokana na matokeo mabovu.

-BBC