Ndoa ya Gloria Muliro ilipovunjika alimlaumu mume wake na kusema kuwa aliyekuwa mume wake alikuwa na mpango wa kando.
Muliro alisema kuwa alikuwa na uhakika kuwa mume wake alikuwa na mpango wa kando kwani rafiki zake walikuwa wanamwambia lakini alikuwa anajifanya kutoskia mambo yao.
Vilevile, Omba alipoulizwa ni somo lipi alipata alipokuwa kwenye ndoa yake na Gloria alisema kuwa wanawake wanafaa kuwa wanazingatia maisha yao na mume wao na si kusikiliza mambo ya watu kwani jambo hili linaweza kuharibu ndoa.
''Alichokuwa nacho Gloria kila mwanamke anacho. Wakati mwingine unafaa kuzingatia mume wako na si kusikia mambo ya watu wengi kwani tabia hii itaharibu ndoa yako.'' Omba
Baada ya ndoa yake Omba na Gloria Muliro kuvunjika, bwana huyu alioa mke mwengine na kwa sasa anaishi maisha mazuri na mke wake.