'Je wakumbuka tulichokubaliana?' Ruto amuuliza Uhuru leo ikiwa birthday yake!

uhuru.birthday
uhuru.birthday
Hii leo ikiwa maadhimisho ya miaka 58 tangia rais wa nne wa jamhuri ya Kenya, mheshimiwa Uhuru Kenyatta azaliwe, wakenya wengi wamechukua fursa hiyo kumtakia heri njema akiwemo naibu wake, William Ruto.

Ruto kupitia mtandao wa Twitter, alimtumia bosi wake ujumbe mfupi akimtakia baraka tele.

Hata hivyo, katika ujumbe wake, alimsifu Uhuru kwa kuwa mtu aliyempa yeye na mamilioni ya wakenya msukumo mkuu kwa kuwa rais mchanga zaidi nchini.

Ujumbe huo haukuishia hapo kwani alimalizia kwa kumkumbusha mkuu wake kuwa anangoja siku watakapostaafu ili wawili hao wafanye walichokubaliana.

Ruto aliandika,

Happy birthday to my friend & Boss H.E. Uhuru Kenyatta. You are a great inspiration to me, Jubilee leadership and millions of Kenyans as the youngest President we've ever had. As we age, I look forward to what we agreed on to do when we retire. Remember? Ubarikiwe mpaka Ushangae!

Ujumbe huo ulizua maswali mengi miongoni mwa Wakenya huku wengi wakijiuliza iwapo Ruto anapanga kustaafu pindi tu hatamu ya rais Kenyatta itakapoisha, mwaka wa 2022.

Soma baadhi ya ujumbe.

Donald: You are retiring with the boss? I thought you are in the ballot for 2022?

Migwi: Tuambie kenye Mliagree

Prince Kelvin: Unaretire?

Ronoh: Your promises all seems null and void,where are the jobs for the youths? Where are the mighty Stadiums