Jimbo la Samburu latenga milioni 255 za kukabiliana na virusi vya corona

Capture-87
Capture-87
Shilingi milioni 225 zimetengwa na gatuzi la Samburu kwa minajili ya kufanikisha vita dhidi ya virusi hatari vya corona. Mpango huo unafanikishwa na shilingi milioni 228 kutoka uongozi wa kaunti huku serikali kuu ikichangia shilingi milioni 27.

Mkuu wa fedha katika kaunti hiyo Dorcas Lekisanyal amesema agavana Moses Lenolkulal ashateuwa kamati ya watu wanane ikiongozwa na  Alex Leseketet ili kuangazia maatumizi ya pesa hizo.

Kamishna wa kaunti hiyo John Korir amesema kutakuwepo na kamati nyingine ya kuangazia mipango nyingine tofauti ya kukabiliana na virusi hivyo hatari.

Lekisanyal amesema ununuzi wa mashine ya ICU na kusambaza chakula kwa familia zilizoathirika kutapewa kipaumbele.

“As at now we don’t have ICU beds, we expect to purchase ICU beds, purchase more personal protective gears for health workers, do more on awareness campaigns and an oxygen plant,” alisema .

Ameongezea kuwa mabwawa ya maji yaliyoaharibika katika kaunti hiyo yote yatakarabatiwa ili kuhakikisha kuwa kuna maji ya kutosha katika Samburu Kaskazini, Samburu Mashariki na Samburu  ya kati.