Jinsi umaskini unavyowasukuma wanaume kuwakodisha wake zao, dada zao kwa watalii

Tourists at the beach
Tourists at the beach
"Kuna haja gani kumtajirisha mwanamke mwingine ila wangu hana kazi ?" James Kimani ambaye hufanya kazi ya kuwaongoza watalii, alisema baada ya mtalii kumwagiza amtaftie mwanamke wa kuvinjari naye kwenye likizo yake huku Kenya.

Aidha, Kimani alikiri kwamba mtalii huyo ni mkwasi kupindukia baada ya kumwona akiwafadhili marafiki zake watano na alitaka hata familia yake ifaidike.

Mzungu huyo alitaka kidosho wa kuburudika naye katika likizo yake huku Kenya.

"Baada ya kuwaza, kwa kweli nina mwanamke mrembo, mwembo mzuri mweusi. Ni dadangu mdogo ambaye hajaolewa na ana nidhamu ya hali ya juu. Nitamleta kesho," Kamau alisema.

Kwa hakika Kamau alikuwa akisema kuhusu mke wake ambaye wameoana kwa mwongo moja sasa.

Jioni ya Agosti 2018, alirejea kwake na kumrai kuhusu huo wito.

"Mpenzi wangu, mwanaume huyo ni Mjerumani. Nitakuongoza kwake kesho. Ila kila nitakacho wewe ni kuiga kuwa dadangu ili asishuku na mhakikishe kwamba umempa haja yake yote. Atakapokulipa, tutahitaji hizo fedha kulipa karo za wanawetu wawili," alisema.

Mkewe alikubali na ikawa desturi yao. Kila mara Kamau humsakia wageni wenye hela ili nao wafaidhike.

Mwanamke huyo hutia mfukoni kitita cha shilingi 40,000 kila mwezi kutoka biashara hiyo.

"Bado tunapendana sana, tungali kwenye ndoa pia na tunakuza familia pamoja, Kamau alisema.

Hivi maajuzi, Kamau amempeleka kwa Mwuastralia moja na pamoja na mkwewe wamekuwa mbali kwa majuma mawili.

Kamishina wa polisi katika kaunti ya Kilifi amekiri kwamba mambo hayo hutendeka.

Alisema kwamba kumekuwa na kesi nyingi kuhusu mwanamke mmoja aliye na wanaume wawili. Aghalabu wanaume hao huwa mzungu na Mkenya.