Mwanakimikakati wa mawasiliano ya kidijitali Dennis Itumbi ni miongoni mwa maafisa watano katika kitengo cha mawasiliano ya ris kupoteza kazi zao baada ya tume ya utumishi wa umma kuzifutilia mbali nafasi zao .
Itumbi alikuwa mkurugenzi mkuu aliyesimamia mawasiliano ya kidijitali .
Nafasi nyingine zilizofutiliwa mbali ni mkurugenzi mkuu wa mawasiliano anayesimamia hafla , mkurugenzi mkuu anayesimamia uandhishi wa hotuba na afisa mkuu wa mawasiliano .
Nafasi hizo nyingine zilikuwa zikishikiliwa na James Kinyua, Erick Ng'eno, David na John Ndolo. Katika maelezo kumhusu katika twitter ,Itumbi amejieleza kama mfungaji wa nguruwe . Kupoteza kazi yake kumejiri wiki hii ambayo alishehekea siku yake ya kuzaliwa . Itumbi amekuwa katikati ya kesi inayohusisha barua iliyokuwa na madai ya njama ya kumuua naibu wa rais William Ruto .