Jombi atumia gundi kumfunga mkewe sehemu za siri

Kisa cha kushangaza kimefanyika nchini Qatar katika familia moja ya jombi na ambaye kwa muda mrefu amekuwa akimshuku na kuwa na wivu wa kimapenzi uliopita mipaka kwa bibi yake.

Hii ni hali ambayo hutokea mara kwa mara katika mahusiano mengi miongoni mwa watu ila kalameni huyu alizidisha mno.

Soma mengine hapa.

Alikuwa anajiandaa kuenda safari yake ambayo ilitakiwa ichukue siku kadhaa wakati na ambapo alishtuka ghafla kuona bibiye  amechapisha picha inayoonyesha kisigino katika akaunti yake maridhawa ya Facebook. Katika nchi ya Qatar, inaaminika kuwa ni mwiko kwa mwanadada kuonyesha sehemu kama hii na nyinginezo  kwa watu wengi hususan kwenye mitandao ya kijamii kama Facebook.

Itikadi hizi huwabana wanawake na huwa wanatakiwa kila mara kuhifadhi na kuwa wakweli katika jamii. Alizidi kupekua katika mtandao huu na kuona bibi yake pia ameridhishwa na kufurahishwa na picha iliyochapishwa na binamu yake wa jinsia ya kiume.

Alikasirika bwanake na akachukua gundi na kwa kutumia nguvu nyingi akaitumia kuzifunga sehemu zake za siri mke wake. Hali kadhalika alimburuza bibiye kortini ili aweze kuyajibu mashtaka ya kuonekana anasaliti penzi lao na binamu yake wa jinsia ya kiume.

Jaji alihoji kuwa kosa hilo kweli lilikuwa na uzito na kuna uwezekano mkubwa likamsababishia kuzongwa na mawazo na kumkosesha amani. Korti hiyo ilimtoza bibi yake kiasi cha hela kilicho sawa na Kshs 1000  na akaachiliwa huru.