Jubilee hakitamsimamisha mgombeaji katika uchaguzi mdogo wa Msambweni ODM-Tuju

TUJU
TUJU
Chama cha Jubilee hakitamsimamisha mgombeaji katika uchaguzi mdogo wa Msambweniu  .

Kiti hicho kiliachwa wazi baada ya kifo cha   Suleiman Dori wa ODM.

Jubilee imesema kwa sababu ya ushirikiano wake na ODM hakitaweza kuwa na mgombeaji katika uchaguzi huo .

Chama hicho kimesema taifa kwa sasa linapitia  mambo mengi ikiwemo ushauri wa jaji mkuu David Maraga   kwa rais Uhuru Kenyatta kulivunja bunge .

" Kwa sasa nchi inapitia mengi na tunahitaji ukomavu  ili kuyashughulikia  ikiwemo kuziba mianya   katika mirengo ya kisiasa’. Amesema  katibu mkuu wa chjama hicho Raphael Tuju

Ameongeza ‘ Uamuzi huu umetolewa kwa wakati ufaao ili iwapo kuna mgombeaji wa Jubilee aliyetaka kiti hiki basi awe na njia mbadala za kugombea’

Wakaazi  wa eneo bunge hilo watamchagua mbunge mpya disemba tarehe 15  baada ya uchaguzi huo kuahirishwa kwa sababu ya janga la corona .