Kupitia mawakili wake Junet amesema matamshi hayo ya Khalwale yamemsababishia fedheha na usumbufu na kumpa hofu kando na kumsababishia mawazo .
Junet amesema Khalwale, alipokuwa Busia kwa mkutano wa hadhara mapema mwezi huu alidai kwamba Junet amelipwa pesa za shirika la Kemsa ambazo zilifaa kutumiwa kupambana na janga la corona nchini
Khalwale aliongeza kwamba mwakilishi wa akina mama wa Homabay Gladys Wanga aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya fedha ili kufanikisha malipo hayo .
Kulingana na mawakili hao , Khalwale alimtaka rais Uhuru Kenyatta kumfuta kazi wazii wa Afya Mutahi Kagwe kwa kuruhusu pesa za Covid 19 kulipwa kwa katibu mkuu wa chama cha Jubilee Raphael Tuju na Junet
Mawakili hao wamesema iwapo khalwale hatoomba msamaha na kutekeleza masharti yao katika siku tatu zijazo wataanzisha utaratibu wa kumfikisha kortini .