Baada ya karibu mwezi mmoja wa patashika kuhusu kutengana kwa Diamond na Tanasha, kimezuka kipya kwamba huenda msaani mwingine TZ Harmonize ambaye awali alikuwa katika lebo ya WCB ameachana na mke wake Sarah . Hii ni baada ya wawili hao kukoma kumfuata kila mmoja katika insta huku wadau wakipiga vijembe kwamba huenda kila mmoja amemlisha mwenzake bonge la Block .
Ushahidi pia umezuka kuonyesha kweli hakuna kati yao anayemfuata mwenzake katika instagram jambo linalozidisha uhalali wa uwezekano wao wa kuachana .
Harmonize kwa sasa anazidi ku promoti wimbo wake mpya na hajasema lolote kuhusu uwezekano wa kutengana na Sarah .
Sarah hata hivyo huenda ametoa taswira ya mambo yalivyo kwa ujumbe fiche aliouweka katika insta story yake na kusema ;
“SHE’S IS BROKEN BECAUSE SHE BELIEVED. HE’S OK BECAUSE HE LIED.”