Kasuku nje ndani kimya: Sudi, Wako hakusema neno hata moja bungeni mwaka wa 2019 – Mzalendo

Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi  hakusema lolote   bungeni mwaka wa 2019,  imeonyesha  ripoti iliyotolewa na shirika la mzalendo.

Kulingana na tathmini ya  ripoti  za hapo awali, Sudi amedumisha sifa yake hiyo ya kutosema lolote bungeni tangu mwaka wa 2017. Mbunge huyo ni mtetezi mkubwa wa naibu wa rais William Ruto  na amekuwa  akitoa maoni kuhusu masuala ya kisiasa

Ripoti hiyo imeonyesha kwamba  seneta wa  Busia Amos Wako  hakuzungumza  katika seneti  mwaka jana  pamoja na viongozi  wengine walioteuliwa

Viongozi hao ni  miongoni mwa wajumbe 25  katika seneti na bunge la  taifa  ambao wametajwa kwa  utendakazi mbovu  katika kipindi hicho. Seneta wa Kajiado Philip Mpaayei,  wenzake  wateule  Christine Zawadi  na  Mercy Chebeni  walitajwa kwa utendakazi adimu.

Seneta  Ledama Ole Kina (Narok)  alitajwa kama mchapakazi zaidi katika seneti.

Alifuatwa na Moses Wetangula (Bungoma), Aaron Cheruiyot (Kericho), Ochilo Ayako (Migori)  na  Getrude Musuruve (Mteule).

Katika bunge la taifa mbunge wa Mumias Mumias West John Naicca; Samuel Arama (Nakuru West); James Gakuya (Embakasi North); George Aladwa (Makadara); Abdi Shurie (Balambala)  ni miongoni mwa waliotajwa kwa utendakazi mbovu  katika bunge na mijadala

Miongoni mwa waliotambuliwa kwa uchapakazi mzuri katika bunge ni  Millie Odhiambo (Suba North), David Ole Sankok

( Mteule ), Wilberforce Oundo (Funyula)  na Robert Pukose (Endebess).