Kaunti ya Taita Taveta imewasilisha ombi jipya katika mahakama kuu ya Voi

Kaunti ya Taita Taveta imewasilisha ombi jipya katika mahakama kuu ya Voi ikitaka kutupiliwa mbali kwa kesi iliyowasilishwa na wafugaji wa ngamia wakipinga agizo la gavana Granton Samboja la kufurushwa kwa mifugo wao.

Wakili wa kaunti hiyo Edwin Chahilu anasema kesi hiyo haina msingi kwani wafugaji hao bado wanaendelea kukiuka haki za wakulima.

Jaji wa mahakama hiyo Farah Amin atatoa uamuzi wa ombi hilo Disemba 21.

Solomon Muingi Junior