Kenya na Tanzania zakubaliana jinsi ya kuwapima madereva wa masafa marefu

LnnBfDCa
LnnBfDCa

Kenya na Tanzania hatimaye imekubaliana jinsi ya kuendesha shughuli ya kuwapima madereva wa masafa marefu baada ya wiki mbili za vute ni kuvute kuhusiana na upimaji wa madereva hao.Wawakilishi wa serikali kutoka kwa mataifa yote mawaili walikutana ili kutafuta njia mwafaka ya kutatua mzozo ambao umekuwa ukiyumbisha biashara katika mataifa husika .

Waziri wa Uchuguzi na usafiri nchini James Macharia na mwenzake kutoka taifa la Tanzania Isack Kamwelwe walikutana katika mpaka wa Namanga na kujadili hatua madhubuti za kutia kikomo kwenye mvutano ambao umekuwepo.

Mazungumzo baina ya mawaziri hao wawili yanajiri siku chache tu baada ya viongozi wa mataifa hayo mawili kuzungumza ili kutatua mvutano huo.

Mkutano huo ulichukua saa sita huku ikidaiwa kuwa palikuwepo na makubaliano kutoka pande zote mbili ya jinsi yua kuendesha shughuli hiyo.

Macharia alisema kuwa Kenya na Tanzania ni lazima izike tofauti zake katika kaburi la sahau na kuangazia namna ya kufufua sekta ya biashara ambayo imeathirika pakubwa.

“Kenya and Tanzania are trade partners, recording a turnover of more than $500 million (Sh53 billion) annually. We have reached an agreement that Tanzanian and Kenyan drivers will be subjected to the WHO standard Covid-19 testing in their territories and issued with clearance certificates,” amesema  Macharia.