Mwakilishi wa kaunti wa Mlang Kubwa Patricia Mutheu amejipata pabaya baada ya polisi kumshambulia kwa rungu na makonde katika jengo la city hall .
Patricia alikuwa miongoni mwa wawakilishi wa kaunti waliokuwa wameenda City Hall kumpa spika wa bunge la kaunti Beatrice Elachi notisi ya kutaka kumfurusha afisini .
Baada ya wawakilishi wenzake kufurushwa kutoka jengo hilo , Mutheu alijipata pekee yake na polisi hawakumsaza kwani walimshambulia na kumpa kipigo kibaya .