Kifo hakichagui!Mpiga picha wa Raila afariki jijini Nairobi

Raila.Anne.Kamoni.696x322
Raila.Anne.Kamoni.696x322

Aliyekuwa mpiga picha wa kampuni ya Nation Media Ann Kamoni na pia mpiga picha wa kiongozi wa chama cha ODM bwana Raila Odinga amefariki.

  

Ann Kamoni alikata kamba Jumapili katika hospitali ya Coptic jijini Nairobi.

Mmoja wa wanahabari wenzake Ann aliandika ujumbe ufuatao kwenye mtandao wa kijamii wa whatsaap.

“SAD STORY FOR ANN KAMONI, ONCE AN INNOCENT, LOVING, KIND-HEARTED, BEAUTIFUL, HARD-WORKING YOUNG GAL BEFORE SHE STARTED CLUBBING,”

Ujumbe mwingine ulitoka kwa Junet Mohamed ambaye alindika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii na kusema,

“Her name, like many of her kind, only appeared on papers as a credit on a photo. I met her fighting addiction. She once broke down at Orange House. She had waned, and it showed. That she fought till now only showed her dogged determination, to win. Sad she lost,”

Zaidi ya hayo,Junet alisema kuwa binti huyu amewacha mtoto mmoja wa kike.

Mkubwa wa mawasiliano wa chama cha ODM bwana Philip Etale aliandika ujumbe wa uhakikisho wa kifo chake Anne Jumatatu lakini hakueleza zaidi ni nini haswa kilicho muua binti huyu.

“MAY YOU REST IN THE ARMS OF THE LORD WHO FORMED YOU FROM THE DUST OF THE EARTH. MY FRIEND ANN KAMONI, MAY CHRIST WHO DIED FOR YOU ADMIT YOU INTO HIS GARDEN OF PARADISE,” Alisema.

Huu ndio ujumbe wao wanahabari waliokuwa wakifanya  kazi na Anne.