Kifungo cha Wema Sepetu kinamtesa zaidi Aunty Ezekiel

sepenga
sepenga
Inaingia siku ya 3 sasa baada ya mahakama Hakimu Mkazi Kisutu Tanzania kumtia nguvuni na kumfunga nyota wa filamu Wema Sepetu. Rafiki wa karibu Aunty Ezekiel ambaye pia ni mwanamitindo na muigizaji wa filamu za bongo amechapisha picha kadhaa katika mitandao ya kijamii akionekana kuumizwa zaidi na tukio hilo.

Pata Uhondo kamili hapa:

Aunty Ezekiel anamtakia Wema Sepetu usiku mwema akiwa gerezani:

"G9t My Love........Inshaalah" Alisema Aunty Ezekiel.

https://www.instagram.com/p/By5g-7qgeUM/

Wema amefungwa kwa sababu ya tuhuma za kupatikana na marijuana na pia kosa la kuchapisha picha za uchi katika mtandao wake wa kijamii. Staa huyu ambaye alikuwa mpenzi wake mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz alisusia vikao vya mahakama hiyo kwa sababu alizozitaja kama kuumwa na hedhi.

Pata Hadithi nyingine hapa:

https://www.instagram.com/p/By2rs6pAVIB/

Kupitia mitandao ya kijamii, Aunty Ezekiel anamhimiza kuwa ipo siku majaribu hayo yatapita na kuwa atazidi kuwa rafiki wake wa karibu.

"Utabaki kuwa Rafiki Mzuri kwangu forever...Inshallah hili Pia litapita." alisema Aunty Ezekiel.

https://www.instagram.com/p/By4frejgnRh/