‘Kill or Capture’:Vita vya siri vya CIA na MI6 nchini Kenya

Kikosi  malum cha Kenya  kilichopewa mafunzo ya kijeshi  na Amerika na kupigwa jeki na habari za kijasusi za  Uingereza ndicho kinachohusioshwa na mauaji ya  tatanishi na  opareshemi za kuwasafiriha magaidi hadi ng’ambo kufunguliwa mashtaka ,uchunguzi umebaini .

Uchunguzi uliofanywa na  Declassified UK, Daily Merverick  nchini Afrika Kusini na The Star  umeonyesha jinsi kikosi hicho cha siri  ambacho kinalipwa na kusaidiwa na CIA kimekuwa kikiwasaka washukiwa wa ugaidi tangu mwaka wa 2004 .

Shirika la ujasusi la Uingereza   MI6  pia lina wajibu mkubwa wa kuwatambua  washukiwa hao  ambao hukamatwa au kuuawa n na pia kufichua maficho yao .

Uchunguzio huo umebaini kwamba kikosi hicho hutumia njia a kisiri katika oparesheniu zake ikiwemo kutumia nambari feki za usajili wa magari  au kuifanya kuwa wafanyikazi wa kutoa misaada  katika oparesheni zinazofanyika kwenye kambi za wakimbizi.

Makomando hao ambao huvamia makaazi ya washukiwa wa ugaidi wanatoka kikosi cha  Rapid Response Team (RRT), ,kundi maalum la  maafisa wa skari kutoka GSU Recce Company.  Kikosi cha  RRT  kiliundwa ,kupewa silaha na kupewa mafunzo ya  kufanya oparesheni za kukabiliana na magaidi  kwenye  oparesheni inayoonekana kufadhiliwa na SHhirika la ujasusi la Amerika CIA  ,uchunguzi ambao siri zake zimefichuliwa umonyesha

Kundi hilo la Kenya linafahamika kwa njia isio rasmi kama   Rendition Operations Team  na lina makomando takriban 60

Programu huyo ya siri ya CIA  iliyoanza mwaka 2004 inaendeshwa na afisa mwandamaizi katika ubalozi wa Amerika jijini Nairobi  lakini hadi sasa mpango wenyewe haujaangaziwa hasa machoni pa umma .

Kwa mujibu wa mahojiano na maafisa kadhaa wa CIA ,Idara ya masua ya kigeni ya marekai na maafisa wa ujasusi wa Kenya ,polisi na  baadhi ya wanachama wa kikosi hicho  imebainika kwamba tangu kuanzishwa ,kundi hilo limehusika kuwakamata washukiwa sugu wa kigaidi  na kufanikisha oparesheni za kuwakata wengine  huku baadhi ya washukiwa hao wakiuawa .