KIND Esther :Passaris aahidi laki mbili kila mwezi kuwasaidia vijana .

Mwakilishi wa akina mama wa Nairobi Esther Passaris
Mwakilishi wa akina mama wa Nairobi Esther Passaris
Mwakilishi wa akina mama wa Nairobi  Esther Passaris  ameahidi kutoa  shilingi laki mbili kutoka kwa mshahara wake kila mwezi ili  kuzipiga jeki biashara zinazomilikiwa na vijana . Akimjibu mtumiaji mmoja wa  twiiter  aliyetaka kusaidiwa kupata kazi  ,Passaris amemwambia hakuwa na nafasi wazi ya kazi lakini alikuwa na uwezo wa kumpa fursa ya kujiajiri .

" Sina nafasi zozote za kazi kwa sasa . Nilicho nacho ni  msaada wa kukupa mkopo wa kukuwezesha ujitegemee’ alisema Passaris ." Ntatoa shilingi laki mbili za mshahara wangu kila mwezi  kwa mawazo mazuri ya kibiashara na watalio na maono au mapendekezo wayatoe katika ukumbi huu .# TwendeKaziKe".