Mwakilishi wa akina mama wa Nairobi Esther Passaris ameahidi kutoa shilingi laki mbili kutoka kwa mshahara wake kila mwezi ili kuzipiga jeki biashara zinazomilikiwa na vijana . Akimjibu mtumiaji mmoja wa twiiter aliyetaka kusaidiwa kupata kazi ,Passaris amemwambia hakuwa na nafasi wazi ya kazi lakini alikuwa na uwezo wa kumpa fursa ya kujiajiri .
" Sina nafasi zozote za kazi kwa sasa . Nilicho nacho ni msaada wa kukupa mkopo wa kukuwezesha ujitegemee’ alisema Passaris ." Ntatoa shilingi laki mbili za mshahara wangu kila mwezi kwa mawazo mazuri ya kibiashara na watalio na maono au mapendekezo wayatoe katika ukumbi huu .# TwendeKaziKe".