Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 28 alipatikana akiwa ameuwawa kikatili nyumbani kwake katika ghorofa la kifahari la Lamuria Garden huko Kilimani, usiku wa Septemba 19, 2018.
Monicah alipatikana huku shingo yake ikiwa imekatwa sikio-kwa-sikio, mikono na miguu yake ikiwa imefungwa na mwili wake kutupwa kwenye tabo la kuoga.
Bomba la maji lilikuwa limefunguliwa huku maji yakiloa mwilini mwake. Dk Joseph Kimani, ambaye hufanya kazi na duka la dawa la serikali, aliiambia korti kuwa kulikuwa na tone la damu katika kaptura (kinyasa) lake, ila mtu hangeweza kusema kwa kutizama tu.
Kaptura hiyo yenye rangi ya kahawia ilikuwa kati ya vitu alivyopewa na polisi ili zifanyiwe uchambuzi. Alisema baada ya uchambuzi, damu kwenye kaptura ililingana na ile ya Monica.
Mwanasaikolojia huyo alimwambia Jaji James Wakiaga kwamba alipokea maonyesho 73 kutoka kwa polisi na vile vile sampuli za DNA na swabs kutoka kwa watu kadhaa.
Daktari huyo alimwambia Jaji James Wakiaga kwamba alipokea maonyesho 73 kutoka kwa polisi na vile vile sampuli za DNA kutoka kwa watu kadhaa.