Mbio hizo maalum zitaandaliwa kesho asubuhi na Kipchoge atasindikizwa na zaidi ya waweka kasi 20. Kipchoge ambaye amekuwa akijitayarisha kwa zaidi ya miezi minne chini ya kocha wake Patrick Sang anasema ana imani ataweza kufaulu.
Timu hiyo inafunzwa na gwiji wa Sevens Waisale Serevi na watawasili Nairobi leo kwa kambi ya wiki moja kabla ya kipute hicho.
Afisa mkuu wa KPL Jack Oguda anajikakamua huku kukiwa na fununu kua huenda ligi hiyo ikasimamishwa kutokana na ukosefu wa fedha.
Oguda anasema taarifa hizo si za kweli na ligi hiyo itaendelea. Ligi hiyo imekua ikiyumbayumba kifedha tangu Sportpesa kusitisha ufadhili wake baada ya leseni yao kufutiliwa mbali.
Baadhi ya vilabu havijawalipa wachezaji wake huku marefa pia wakiwa hawajalipwa.