“Kizungu yako inahitaji quarantine!” Mashabiki wamwambia Ringtone

Uvumi nao unazo habari za msanii wa nyimbo za injili Ringtone na malkia wa Tiktok Azziad Nasenya,wawili hao inasemekana kuwa ni wapenzi baada ya Ringtone kuposti picha yake na Azziad kwenye mitandao ya kijamii.

Ni picha ambayo iliwaacha mashabiki wake wakiulizana maswali yasiyokuwa na majibu, kuna wale walimpongeza Ringtone huku wengi wakidai kuwa Azziad amemchagua Ringtone kwa ajili ya pesa zake wala si upendo.

Hatuna hakika kuhusu uvumi huo lakini tunaweza kusema kuwa msanii Ringtone yupo katika mahaba hata kuandika sentensi vyema hawezi kama vile ilivyoshuhudiwa kwenye mitandao ya kijamii ya Instagram.

"IS IT REALLY A CRIME TO FALL ON LOVE????" Aliandika Ringtone.

Lakini hayo yote asante kwa picha ambayo imesambaa mitandaoni sasa tunajua wawili hao waliungana mikono ili kufanya kazi.

Kulingana na mimi nikijibu swali ambalo Ringtone aliuliza kwenye mitandao hiyo, kibao ambacho kitaenda kutolewa ni kuhusu mapenzi au kuhusu moyo kuvunjwa.

Ata baada ya kumwaibisha msanii Bahati kwa ajili ya kuvaa mavazi ya wanawake, asante kwa msimamizi wake Ringtone kwa maana alimchagulia koti ambalo linakaa la wanawake.

Haya hapa mazungumzo ya mashibiki wake;