KURIA:Uhuru Lazima aondoke Uongozini 2022.

 • Mbunge huyo wa Gatundu kusini amewataka wakaazi wa Nyeri Kumpuuza ‘mlevi’ Murathe

  • Murathe awali amesema Uhuru atasalia uongozini ingawa katika wadhfa tofauti .
  • Kuria amesema Rais anaweza kujizungumzia na hawezi kuwatumia ‘walevi’ kufikisha ujumbe wake .

Siasa za mwaka wa 2022 sasa zimechukua mjadala  mpya baada ya  kuibuka  hoja ya iwapo rais Uhuru Kenyatta ataondoka madarakani  wakati  kipindi chake  kuhudumu  kitakapofika tamati mwaka huo .Jana katika maazishi ya mamake mbunge wa Mathira  Rigathi Gachagua ,naibu wa rais  William Ruto alionekana kutoa matamshi ya kuondoa kabisa mpango wowote wa rais kusalia uongozini kwa kusemakwamba rais Kenyatta ni Mtu mungwana na hatobadilisha katiba ili kusalia uongozini . Hatua hiyo yake sasa pia imewafanya viongozi wengine kuanza kutoa kibwagizo hicho huku mbunge wa gatundu Kusini Moses Kuria  akikariri kauli hiyo kwamba kamwe rais Kenyatta hana mpango wa kuendelea kuongoza baada ya hatamu yake kukamilika katika miaka miwili ijayo.

Kuria pia aliyesema hayo wakati wa  hafla hiyo ya kumzika  Martha Kirigo,  mamake mbunge wa  Mathira Rigathi Gachagua  na aliyekuwa gavana wa Nyeri marehemu   Nderitu Gachagua. Mbunge huyo wa gatundu kusini aliwataka waomboleza kumpuuza aliyekuwa naibu mwenyekiti wa chama cha Jubilee David Murathe  ambaye maajuzi amedai kwamba rais  atasaliamadarakani hata baada ya mwaka wa 2022 katika wadhfa  mwingine wenye ushawishi .

Hofu za kuwepo mpango wa rais kusalia madarakani baada ya 2022 ndizo zinazozua pingamizi na  maswali kuhusu nia ya rais Kenyatta na kiongozi wa odm Raila Odinga hasa kuhusiana na   jopo la BBI na mapendekezo yaliyotolewa na Jopokazi hilo . Kuria alimtaja Murathe kama ‘mlevi’ ambaye walikuwa  wakinywa naye pombe  hadi mwaka  huu alipoamua kuacha pombe ."Mimi nimewacha pombe mwaka huu lakini hiyo miaka mingine tulikua tunakunywa na Murathe’.   Kuria alisema .