Kwaheri Moi: Safari ya mwisho ya Moi yaanza

Baada ya zaidi ya miaka 96 duniani hatimaye safari ya hayati rais mtaafu Daniel Toroitich Arap Moi inafika tamati hivi leo.

Moi anazikwa leo nyumbani kwake Kabarak katika kaunti ya Nakuru. Maombi ya mazishi yanaandaliwa katika shule ya msingi ya Kabarak kabla ya mwili wake kusafirishwa takriban kilomita nne hadi nyumbani kwake atakapozikwa mkabala na marehemu mkewe Lena Moi aliyefariki mwaka 2004.

Maombi rasmi ya kumwombea hayati Moi yaliandaliwa siku ya Jumanne katika uwanja wa kimaaifa wa Nyayo na kuhudhuria marais na viongozi kadhaa wa nchi mbali mbali.